Mgombea urais kupitia chama cha Republican, Donald Trump amepitishwa na chama hicho kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu nchini Marekani utakaofanyika Novemba mwaka huu.
Trump amepata uungwaji mkono na wajumbe kutoka majimbo na wilaya za Marekani katika kura za mchujo wa kumpata mgombea wa nafasi hiyo kupitia chama cha Republican kwenye mkutano mkuu uliofanyika mjini Cleveland nchini Marekani.
Baada ya kuchaguliwa Donald Trump alitoa shukran zake kwa wananchi kutokana na kumuunga mkono kwenye harakati zake za kuwania kiti cha urais wa Marekani.
Kwa upande mwingine gavana wa jimbo la Indiana nchini Marekani, Mike Pence amechaguliwa kuwa mgombea mwenza wa Donald Trump kwenye uchaguzi huo.
Trump: Akiwa kwenye moja ya mikutano yake jijini New York.
Kanda za maonyesho wa gwiji wa muziki wa Reggae Bob Marley ambazo ziliokotwa baada ya miaka 40 kwenye hoteli iliyotelekezwa jijini London zimetengezwa.
Kanda hizo...
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Harmonize amefunguka na kusema kuwa mpenzi wake Sarah ana ujauzito mkubwa na muda wowote anaweza kujifungua.
Harmonize amesema hayo wakati akipafomu...
Klabu ya Atletico Madrid imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Europa ligi baada ya kuifunga Olympique Marseille 3-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika jana.
Magoli ya Atletico yakifungwa na Antoine Griezmann dakika ya 21 na...
Golikipa wa Manchester United, David De Gea ameshinda tuzo ya Golden Glove award katika ligi kuu Uingereza akimshinda golikipa wa Manchester City, Ederson.
Ameshinda tuzo...