Klabu ya Tianjin Quanjian ya China imesitisha dili la kumsajili mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa kutokana na sheria mpya ya usajili itakanza kutumika msimu mpya wa ligi hiyo itakayoanza mwezi Machi.

Mmiliki wa klabu hiyo ya China, Shu Yuhui amesema kuwa sheria ilioanzishwa imekuja kusababisha kalbu za China kusitisha kusajili wachezaji wa kigeni kutokana na wachezaji watatu tu ndiyo watakaonza kucheza kwenye mechi moja.

Klabu za ligi ya China zitaruhusiwa kuchezesha wachezaji watatu wa kigeni kwa kila mechi kwenye msimu mpya utakaoanza mwezi machi mwaka huu.

Sheria hiyo imekuja ili kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni wanaosajiliwa kwenye ligi hiyo kutoka barani Ulaya ili kukuza wachezaji wa ndani ya nchi hiyo.

Hapo awali sheria ilikuwa “4+1”  mana yake wachezaji wanne wa kigeni kutoka taifa lolote na mchezaji mmoja kutoka ndani ya bara la Asia kwenye kikosi.

Klabu hiyo ya Tianjin Quanjian inafundishwa na naodha wa zamani wa timu ya taifa ya Italia Fabio Canavaro.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *